Wednesday, December 5, 2012

MH. CHARLES KITWANGA AFANYA ZIARA YA GHAFLA KATIKA VIWANDA JIJINI KUANGALIA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA KUTUNZA MAZINGIRA.

Mkurugenzi wa Tahmini ya Athari kwa Mazingira (Enviromental Impact Assessment-EIA) wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw.Ignace Mchallo akitoa taarifa fupi kwa waandishi wa habari kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC ambapo amesema Wizara imetoa agizo la kufanya ziara katika Viwanda vilivyopo eneo la Mikocheni na fukwe za hoteli zilizoko katika bahari ya Hindi maeneo ya Manispaa ya Kinondoni kujionea changamoto za uchafuzi wa mazingira katika maeneo hayo ambayo huleta athari kwa jamii kwa ujumla. Katikati ni Mkuu wa Msafara Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga na kulia ni Mkemia Mkuu wa Mazingira katika Ofisi hiyo Bi. Rogathe Kisanga.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya kufanikisha udhibiti wa Mazingira Mhandisi Dr. Robert Ntakamulenga kutoka NEMC akitoa maelezo kwa Naibu Waziri ambapo amesema NEMC imetoa agizo kwa wamiliki wa Viwanda kuhakikisha wanafunga mitambo maalum yakusafisha maji taka yatokanayo na bidhaa wanazozitengeneza hasa zinazotumia rangi kabla ya kuyamwaga katika mifumo ya maji machafu ili kupunguza athari za uharibu wa mazingira.
Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akizngumza na waandishi wa habari kabla ya kuanza ziara ya kukagua Viwanda na Mahoteli yaliyopo maeneo ya fukwe za bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam ambapo amewataka Watanzania kuzijua na kuzifwata sheria za Mazingira ikiwemo sheria ya mwaka 2004 namba 20 inayowataka watu kutunza mazingira yanayowazunguka.
Mwanasheria wa NEMC Bw. Mwanchane Heche akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri kuhusiana na hatua zinazopaswa kuchukuliwa kisheria kwa watu wanaochafua mazingira wakiwemo wanaomwaga maji machafu yenye kemikali zinazoharibu Mazingira kutoka viwandani wakati wa ziara ya kukagua Mto Mlalakuwa uliopo maeneo ya Kawe jijini Dar es Salaam.
Huu ndio Mto Mlalakuwa Kawe Darajani unavyoonekana ambapo maji yake yanaonyesha kuchafuliwa na maji taka yatokayo viwandani.
Mkurugenzi wa Tahmini ya Athari kwa Mazingira (Enviromental Impact Assessment-EIA) wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bw.Ignace Mchallo akifafanua jambo kwa Mh. Charles Kitwanga wakati wa ziara hiyo sambamba na jopo la waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali.
Eneo la Mto Mbezi lenye mgogoro kufuatia kuzuia mtiririko wa maji ya Mto huo ambalo limenunuliwa na mtu Binafsi anayefahamika kwa jina la Robert Mgishwagwe ambaye kila anapofuatwa na vyombo husika kumtaafiru kwamba eneo hilo haliruhusiwi kujengwa amekuwa akikaidi na kudai kwamba yeye ni mfanyakazi wa Usalam wa Taifa. Kitendo cha kuweka Kifusi na kukisawazisha katika njia ya maji ya mto Mbezi na kimesababisha Daraja lililopo kando ya eneo hilo kuvunjika kila mara na kusababisha usumbufu kwa wananchi.
Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akikagua eneo la kiwanja cha mtu huyo kinachosababisha usumbufu kwa wananchi na kutoa agizo kwa Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira pamoja na maafisa wa Wizara yake kuhakikisha hatua za kisheria zinachukuliwa mara moja dhidi ya mtu huyo.
Msafara wa Mh. Charles Kitwanga ukiwasili eneo la Viwanda Mikocheni jijini Dar es Salaam tayari kwa ziara ya Ukaguzi.
Pichani Juu na chini ni Mheshimiwa Naibu Waziri Charles Kitwanga (katikati) kipata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kuratibu Miradi wa kiwanda cha MM I Steel Bw. Lawrance Manyama (kushoto) wakati alipofanya ziara rasmi kuangalia changamoto za uharibu wa mazingira unaotokana na Viwanda na Mahoteli. Kulia ni Mhandisi Dr. Robert Ntakamulenga.
Mh. Charles Kitwanga katika ziara ya ghafla katika kiwanda cha MMI Steel akikagua moja ya shimo la maji taka katika kiwanda hicho ambapo ameuagiza utawala wa Kiwanda hicho kuingia katika makubaliano maalum na NEMC katika siku chache zijazo kuhakikisha wamefunga mitambo maalum ya kutibu majibu taka yenye kemikali za kutoka viwandani mwao kwa kiwango kinachokubalika kitaifa.
Meneja Mkuu wa kiwanda cha TANPACK TISSUES Ltd. Bw. Rajesh Shah akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri Mh. Kitwanga kuhusiana na kiwanda chake kuwa na mikakati ya kuhakikisha maji taka yatokanayo na uzalishaji kiwandani humo hayataleta madhara kwa jamii.
Mh. Charles Kitwanga akikemea vikali tabia ya uchelewashwaji wa maagizo yanayotolewa na Serikali wakati wa ziara yake katika Kiwanda hicho sambamba na viongozi wa NEMC.
Meneja Mkuu wa kiwanda cha TANPACK TISSUES Ltd. Bw. Rajesh Shah akimuonyesha Mh. Naibu Waziri Charles Kitwanga sehemu maalum ya kuchujia maji taka yanayotoka katika kiwanda hicho.
Meneja Mkazi wa Kampuni ya BIDCO inayotengeneza mafuta ya kula na sabuni Bw. Hemal Shah akimuogoza Mh. Kitwanga kukagua tenki linalohifadhi uchafu baada ya kutengeneza sabuni ambao pia husafishwa kitaalamu kupunguza kemikali zilizomo ndani yake.
Pichani Juu na Chini Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akikagua matenki hayo wakati wa ziara hiyo aliyoambatana na wanahabari pamoja na viongozi wa NEMC.
Maafisa wa Wizara, NEMC na baadhi ya wanahabari wakiangalia taratibu zinazopitiwa kupitisha na hatimaye kusafisha maji taka ya viwanda kabla ya kwenda kuyamwaga katika maeneo ya wazi.
Naibu Waziri Mh. Kitwanga akitoa agizo kwa Uongozi wa BIDCO wakati wa ziara ya kukagua viwanda mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh.Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhitimisha awamu ya kwanza ya ziara ya kutembelea viwanda vya jijini Dar es Salaam ambapo amesema ziara hiyo imempa nafasi ya kujionea hali halisa ya viwanda vya jijini na kugundua kuwa vingi havina mitambo ya kusafisha maji machafu yanayokwenda kumwagwa kwenye mito na kushuhudia kuwa vingine havina viwango vya kupeleka maji taka yake kwenye mtandao wa maji taka ya DAWASCO na kuwataka kufikia viwango vinayokubalika na mazingira yetu.
Msafara wa Naibu Waziri wa Nchi kwenye Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mh. Charles Kitwanga ukiondoka mara baada ya kumaliza ngwe ya kwanza ziara ya Kukagua Viwanda kuangalia hali halisi jinsi viwanda hivyo vinafuata kanuni za utunzaji mazingira.

No comments: